Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Sunday, October 7, 2012

Ronaldinho Ang’ara afunga Hat-Trick dhidi ya Figueires katika ligi kuu ya nchini Brazil.


Ronaldo de Assis Moreir


Mchezaji  bora wa zamani wa FIFA mara mbili mwaka 2004-2005  Mbrazili Ronaldo de Assis Moreira  maarufu kama  Ronaldinho  amefanikwa kufunga  magoli matatu  ( hat-trick)  kati ya  magoli  6-0 klabu yake   ya   Atletico Mineiro  ilipoilaza klabu ya Figueires  kwenye mchezo wa ligi  kuu ya nchini humo.

Ronaldinho  alijiunga na klabu hiyo  mwaka huu akitokea klabu ya  Flamengo  alianza kufungua  mvua hiyo ya magoli katika  dk ya  12  kwa  kupiga  mpira  safi nje kidogo ya kumi nane  uliongia kimyan moja kwa moja.

Goli la pili la Ronaldinho lilifungwa katika dk 32  ya mchezo huo na lile la 3 akifunga kwa njia ya penaiti .Magoli mengine yalifungwa na  Mchezaji  River  mara baada ya kupokea pasi maridhawa kutoka  kwa ronadinho  huku goli la 5 likifungwa na bernadi katika dk ya 68  kabla ya   Carlos  Cesar kupigilia msumari wa mwisho  katik dk ya 82.

Kwa matokeo hayo kumeisadia  klabu ya  Ronaldinho kufikisha pointi   na kuwa nyuma  ya vinara wa ligi hiyo   klabu ya  Fluminense  yenye pointi  62 huku   yeye akishika nafasi ya kumi na sita kwa kufunga magoli nane.

No comments:

Post a Comment