Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Monday, October 22, 2012

kila la kheri vijana wetu.



kikosi cha serengeti boy

Timu ya taifa ya chini ya umri wa miak 17 maarufu kama serengeti boys imeingia kambini rasmi kujiandaa  kwa ajirir ya mchezo wa raundi ya mwisho kabla ya kuelekaea katika michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika kwa vijana  wa chini ya umri wa miak 17.

timu hiyoi ambayo iko chini ya kocha  Jakob  michelsen imeingia kambini ikwa na idadi ya wachezaji  25   ambapo katika michezo yake ya raundi ya 3 timu hiyo itacheza na mshindi kati ya Congo Brazzaville na Zimbabwe ambapo tayari Congo Brazzaville imefanikiwa kupata ushindi wa ugenini wa mabao 2-1. Mechi ya marudiano itachezwa jijini Brazzaville kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu.

 

baadhi ya wachezaji wa  Serengeti Boys wafanya mazoezi ya viungo.

 huku katika michezo hiyo timu ya taifa ya serengeti boys itaanzia nyumbani katika mchezo utakaofanyika Novemba 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, wakati mechi ya marudiano itachezwa wiki mbili baadaye.

kwa mujibu wa  Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesema liko  katika mikakati ya kuhakikisha Serengeti Boys inapata mechi mbili za kirafiki za kimataifa kabla ya kumvaa mshindi kati ya Congo Brazzaville na Zimbabwe. Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitafanyika Machi mwakani nchini Morocco.

No comments:

Post a Comment