Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Sunday, October 7, 2012

Falcao: Natumani ipo siku nitaenda kucheza ligi ya uingereza na kuwa miongon mwa wafungaji kwani nimekuwa nikifuatilia tangu nilipokuwa mtoto






                   Radamel Falcao               

Mshambuliaji  wa kimatifa  Radamel Falcao anayecheza  katika klabu ya Atletico  Madrid  ameonesha nia  yake ya kutaka kucheza mpira katika ligi kuu ya nchini  Uingereza kama alivyofanya  mkolombia mwenzake  Faustino  Asprilla  aliyekuwa anacheza katika klabu ya new castle  united  kwenye miaka ya  1996–1998.
Radamel Falcao 26, aliyeonesha kipaji chake kwa kuifunga klabu ya chalsea kwenye mchezo wa kuwania Europian  super cup  amesema  kucheza kwake katika ligi ya England   kutampa furaha moyon mwake kwani tangu alipokuwa mdogo amekuwa akifuatilia ligi hiyo  tangu zama za mkolombia mwenzake Asprilla aliyekuwa akicheza new castle united.

Faustino Asprilla


Akiwataja baadhi ya wachezaji waliokuwa wakimkuna kichwa  kama vile  Roy keane,Eric cantona (Gianfranco ) wote wa kutoka klabu ya Manchester united  mchezaji huyo amesema Nimekuwa nikiifatilia ligi ya England kupitia television tangu nilipokuwa  mdogo  huku kivutio kikibwa zaidi kilikuwa kwa Mkolombia mwenzake  Faustino  Asprilla.
Ikumbukwe kuwa mchezaji huyo amekuwa akihusishwa na klabu  mbalimbali za uingereza  moja wapo ni mabingwa wa ulaya klabu ya chalsea ambayo kwa mujibu wataarifa klabu hiyo imetenga  £45 millioni za kumsajiri mshambuliaji huyo.
              

No comments:

Post a Comment