Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Thursday, October 4, 2012

Kocha Roberto mancini amesema alifanyia kazi tatizo linaloikumba klabu yake hadi kushindwa kuibuka na ushindi katika uwanja wake wa nyumbani.

kocha wa manchester City Roberto Mancini.

Kufuatia klabu ya Manchester  city  kulazimishwa  sare ya  kufungana  goli 1-1  katika uwanja wake wa  nyumbani   dhidi ya mabingwa  wa ujerumani  klabu ya   borusia  Dortmundi  katika michuano ya  ligi ya mabingwa jumatano hii kocha wa klabu hiyo  muitaliano  Roberto  Mancini  amekiponda kiwango kilichoonesha na klabu yake na kusema kuwa walicheza chini ya kiwango  na  kuahidi kutatua  tatizo lililopo sasa hivi.
Kocha huyo amesema  wanahitaji kubalidikia na kucheza kwa juhudi ili wawe kama wapinzani  wao Borrusia dortmundi na kuongeza kuwa michuano ya UEFA ni migumu nanitofauti na michuano mingine  na hakusita kumwagia sifa kemkem golikipa Joe  Hart kwa juhudi yake ya kuokoa  mipira ambayon ingeiweka pagumu klabu hiyo yenye pointi moja katika kundi hilo.

Katika mchezo huo klabu ya  Manchester city ilionekana kuzidiwa kimaarifa na wajerumani hao  kama vile kwenye safu ya kiungo kulionekana kupwaya zadi na hivyo kuwapa mda mzuri wajeruman  hao wa kutawala safu  na kuchezea mpira kama wako nyumbani kwao.

 

   

 

No comments:

Post a Comment