Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Thursday, October 25, 2012

AFCON 2013, Je zambia itatetea ubingwa....?

Zimebakia takribani siku 86 kwa wapenzi wa soka barani Afrika na duniani kuelekea Bondeni kwa mzee Mandela ambako michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika (AFCON) itafanyika huku ile droo ya makundi imekwishafanyika na kushuudia mabingwa wa kombe hilo timu ya taifa ya Zambia ikiwa kundi moja na timu ngumu ya Nigeria,burkinafaso pamoja na Ethiopia.

 


Makundi ya timu zitakazoshiriki michuano hiyo ni

Group A: South Africa, Morocco, Cape Verde, Angola

Group B: Ghana, Mali, Niger, DR Congo

GROUP C: Zambia, Ethiopia, Burkina Faso, Nigeria

Group D: Ivory Coast, Togo , Algeria, Tunisia

Katika makundi haya kundi linalotazamiwa kuwa  gumu ni kundi D pamoja na kundi B kwani makundi haya mawili yamebeba timu kongwe na ngumu.kwa mfano kundi D lenye timu za ivory cost ambao walikosa ubingwa huo mwaka huu kwa kufungwa na timu ya Zambia kwa njia ya peniti.


Timu ya taifa ya Afrika kusini

 Timu ambayo inayotazamiwa kuleta upinzani katika kundi hili ni timu ya taifa ya Tunisia,pamoja na hawa Algeria ambapo kwa kawaida timu hizi za mafia za kiarabu zimekuwa zikileta ugumu kwa timu hizi za asili za kiafarika.

 Katika kundi B hili nalo ni kundi gumu zaidi kwani limekutanisha timu ngumu kama Mali,DR Congo ambapo timu kama ya Ghana inauchu mkubwa sana wa kutwaa taji hili.

timu ya taifa ya zambia

Bingwa mtetezi yeye katika kundi lake si gumu sana pengine ukilinganisha na kundi A kwani Zambia hatapata upinzani mgumu kama atakaopata  Ghana itakapocheza na Mali au congo ila ugumu utakuja pindi Zambia atakpocheza na timu ya taifa ya Nigeria 

 

Hata Ethiopia,Burkinafaso, si timu za kubeza kwani nazo zimejianda vya kutosha katika kuelekea huko afrika kusini. 

Didier Drogba.

Swali je, Zambia itatetea ubingwa wake,Didier drogba yuko tayari kuona anakwenda kusitaafu soka bila hata ya kulipatia taji taifa lake la ivory cost…?

No comments:

Post a Comment