Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Tuesday, October 30, 2012

kocha wa timu ya taifa ya zambia Herve Renard amesikitishwa na kitendo cha timu ya taifa ya kenya kumteuwa Henry Michel kama kocha wa timu ya

kocha-Herve Renard

Kocha wa timu ya taifa ya Zambia  mfaransa  Herve  Renard  ameshangazwa  na kitendo  cha timu ya  taifa ya Kenya Harambee  stars  kumteuwa mfaransa  mwenzake  Henry  Michel  kama kocha mkuu wa timu hiyo

Kocha huyo amesema Henry  Michel  si chaguo sahihi  kwa  timu ya taifa ya Kenya  kwani ni vema  kwa timu ya taifa ya kenya kupata kocha ambaye ataendana na wachezaji ikiwemo kuwapa hamasa ya kucheza mpira

 “Kenya  ina kila kitu  lakini  nafikiria ya kwamba imekosea kuchagua kocha ambaye  hana atauwezo  wa kuisaidia timu  kwani Henry  Michel  rekodi yake ni mbaya    hivyo   kenya inahitaji    kocha   ambaye anauwezo mkubwa wa kufundisha na sio Henry”,Alisema  kocha Herve Renard.

Herve  Renard ni kocha  mwenye  mafanikio makubwa katika timu ya taifa ya Zambia kwani amefanikiwa kutwaa  kombe la mataifa ya afrika maarufu kama (AFCON)  mwaka huu wa 2012 akiifunga timu ya taifa ya ivory cost kwa mikwaju ya penaiti,pia kocha huyo amefanikiwa tena kuipeleka Zambia katika michuano hiyo itakayofanyika huko nchini Afrika kusini mapema mwakani

 

No comments:

Post a Comment