Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Friday, October 12, 2012

Hivi ndivyo vita ya uhasama wa mpira ulivyoanza kati ya zambia vs uganda ambao umedumu mpaka kizazi cha leo..! je zambia watafanikiwa kuingia fainali ya michuano ya kombe la mataifa afrika..?



Herve Renard -Kocha wa zambia

Timu   za taifa  za  Zambia  na Uganda  zimekutana  takribani mara kumi na tano katika michuano mbali mbali  kama vile kufuzu kucheza  kombe la dunia,michuano ya afrika mashariki na kati maarufu kama  challenge cup  ambapo timu ya taifa ya Uganda ndo inaongoza kwa kushinda  mechi 8 kati ya 15 hali ya kuwa timu ya taifa ya Zambia imeshinda mechi 7

Ushindani wa timu hizi mbili ulianza mwaka 1973 katika michuano ya afrika mashariki na kati  maarufu kama challenges cup ambapo Uganda walikuwa wenyeji  wa michuano hiyo

vijana wa zambia wakipasha kuelekea mchezo dhidi yaa uganda

Katika mashindano hayo timu hizo zilifanikiwa kutinga fainali  ambapo mchezo wa kwanza zilitoka sare ya kufungana goli 1 kwa 1 na ndipo mchezo wa marudiano ukapangwa kuchezwa siku  inayofuata  ambapo timu ya taifa ya Uganda ikafanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 kwa kutoka nyuma huku magoli hayo yakifungwa na Polly Ouma pamoja  na  Stanley “Tanker” Mubiru.

 

Mwaka 1974 timu hizi zilikutana  tena katika michuano ya mataifa ya Afrika kwenye hatua ya makundi huku kundi hilo lilikuwa na wenyenji timu  ya Taifa ya Misri,Ivory cost pamoja kundi hilo kuwa natimu ngumu timu ya taifa ya Zambia ilifanikiwa kusonga mbele kwa kuifunga timu ya Uganda goli moja  kwa bila  wakati wa mchezo wa mwisho wa kutafuta timu itakayoingia  fainali.

 Ushindani huo uliendelea kuzitawala timu hizi mbili za Uganda pamoja na timu ya taifa ya Zambia kuazia mwaka huo wa 1973 hadi 1992.

Bobby Williamson-kocha wa uganda

Mwaka 1977  waweza sema ndio mwaka ambao unahisitoriya  kubwa kati ya Tanzania na Uganda  kwani mwaka huo dio vita baina ya  tanzania na uganda ndio ilitokea

Mwaka huo mashindano ya michuano ya kombe la afrika mashsriki na kati maarufu kama challenges  cup  yalifanyika huko Somalia katika mji wa Mogadishu,nchini Somalia.timu   hizi zilikutana  kwenye mchezo wa fainali

 Katika mchezo huo wa fainali Uganda walifanikiwa kuibuka na ushindi  kwa kuifunga Zambia goli 5-3 kwa njia ya penaiti kwani timu hizo zilimalizika dk 120 zikiwa zimetosha nguvu nguvu  huku shukrani za kipekee zimuende golikipa wa Uganda wakati ule waya  Paul Ssali kwa kuibuka shujaa  kwa kuokoa penaiti mbili za Zambia.

kikosi cha uganda kikiwa mazoezini

Mchezo ambao timu ya taifa ya Uganda hauta usahau ni wa mwaka 1988  ambapo timu hiyo ilikubali  kipigo cha  jumla ya magoli 6-2 katika mchezo wa kuwania kushiriki michuano ya olimpiki yaliyofanyika huko korea.

Mechi ya kwanza ilichezwa Uganda ambapo wenyeji Uganda walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 huku magoli hayo yakifungwa na wachezaji kina Magid musisi pamoja na Ronald Vubya .

 

kikosi cha timu ya taifa cha uganda

Inasemekana timu ya taifa ya uganda ilijichimbia kabri lake kwani kabla ya mechi ya marudiano  mchezaji John Latigo ambaye alikuwa beki wakutegemewa upande wa kulia aliondolewa  kwenye kikosi hicho na kocha Edward senkwangu kutokana na utovu wa nidhamu ambapo mchezaji huyo alitoloka wakati timu hiyo ikiwa kambini kwa ajiri ya kuwakabili wanachipolopolo.

Mchezo wa pili wa marudiano ulichezwa huko Zambia na timu hiyo ya Uganda ilipokea kipigo cha goli 5-1 kutoka kwa vijana hao wa Zambia akiwemo  mchezaji Kalusha Bwalya

kikosi cha timu ya taifa-Zambia

Pia mwaka huo tukio kubwa lilitokea katika medani ya soka dunian kwani ni mwaka ambao wachezaji wa Zambia walipoteza maisha kwa ajari ya ndege walioyokuwa wanasfari nayo kwa ajiri ya kuelekea huko gabon kushiriki michuano  ya kombe la afrika

Miaka iliyofuata yaani mwaka 1989 na 1992 uganda ilifanikiwa kuibuka na ushindi katika michezo iliyocheza na timu ya taifa ya Zambia

Mwaka huo katika kusaka tiketi ya kuelekea afrika kusini kwa ajiri ya miachuano ya kombe la mataifa la afrika wakati wa mchezo wa kwanza timu ya taifa ya Zambia ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila..,Je, Zambia au Uganda  Ni nana yupo tayari kupoteza  mchezo huo   ambao utaipa tiketi kila timu ya kwenda  huko kwa Mandela mwaka 2013.dakika 90 za mchezo ndizo zitakazo amua nani   aende nani abaki.

No comments:

Post a Comment