Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Wednesday, October 17, 2012

RAIS WA SHIRIKISHO LA MPIRA NCHINI SENEGAL,AUGUSTIN SENGHOR AMESEMA HAWEZI KUJIUZURU:



AUGUSTIN  SENGHOR -RAISI SHIRIKISHO LA MPIRA SENEGAL

Raisi wa shirikisho   la mpira  wa miguu  nchini  Senegal  Augustin Senghor  amesema yeye pamoja na kamati ya utendaji ya shirikisho hilo  hawezi kujiuzuru  kutokana  na tukio la vurugu zilizotokea wakati wa mchezo kati ya timu ya taifa ya nchini  senegal walipokuwa wameikaribisha  timu ya taifa ya ivory cost  kwa ajiri ya kuwania nafasi  ya kuelekea afrika  kusini kutakochezwa michuano ya kuwania kombe la mataifa afrika maarufu kama AFCON mwaka 2013  ambapo mchezo huo ulivunjika katika  dk ya 76 hali ya kuwa wageni ivory wakiwa mbele kwa goli 2-0

 

baadhi ya mashabiki wa nchini senegal wakati wa vurugu.

Augustin senghor,  “Sisi tumechaguliwa kwa mkataba wa miaka  minne,bado hatujafikia  hata robo ya malengo yetu tulioazimia kuyatekeleza kabla ya mda wetu kumalizika,hivyo hatuwezi kujiuzuru kutokana na vurugu hizo za jumamosi na hao wanaotaka  sisi  tuondoke madarakani wanapoteza mda wao”.

     Pia raisi huyo amesema  vurugu hizo  za jumamosi zimesabishwa  na mtu mmoja hasiye na mapenzi ya dhati  ya kuendeleza mpira nchini humo ambaye alitoa pesa kwa vijana wafanye  fujo na ikumbukwe  kuwa  siku zilizopita  shirikisho hilo lilimshutumu mchezaji El Hadji Diouf   kuwa ndo chanzo cha vurugu hiyo

El Hadji Diouf


Hatua  hiyo ya shirirkisho kutangaza kuwa hawatajiuzuru  imekuja kufutia mchezaji  El Hadji Diouf kuutaka uongozi uliopo madarakani kujiuzuru mara moja.

No comments:

Post a Comment