Aaron Ramsey |
Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo
Tuesday, November 6, 2012
Klabu ya Esparance yazikimbiza klabu za ulaya katika timu bora mianne za duniani,huku sudani ikiwakilishwa na klabu mbili katika takwamu hizo .
Klabu ya Barcelona |
Shirikisho la kimataifa linalohusiana na masuala ya takwimu na historia ya masuala ya mpira wa miguu duniani (IFFHS )limetangaza takwimu ya timu bora mianne za mwezi wa kumi huku vinara wa ligi kuu ya nchini uhisipania Klabu ya Barcelona ikiongoza kwa kushika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 349 ikifuatiwa na mabingwa wa ligi hiyo klabu yab real madridi wao wakiwa na pointi 290 huku klabu ya boca juniors ikishika nafasi ya 3 kwa kuwa na pointi 276
Licha ya hivyo klabu nazo za afrika zimefanikiwa kuingia katika timu mia moja bora ambapo klabu hizo ni Klabu ya Esperance Tunis ya nchini Tunisia ikishika nafasi ya 61 kidunia kwa kuwa na pointi 148.5 huku kwa afrika ikiwa nambari moja na Al Hilal Omdurman ya nchini Sudani ikiwa na 129 huku ikishika nafasi ya 82
klabu ya Esparance |
Klabu hiyo ya esparance imefanikiwa kuzibwaga klabu toka barani ulaya kama klabu ya Fc Porto yenyewe ikishika nafasi ya 71,Lille 77,Bordeaux79, na New castle 83
Klabu zilizofanikiwa kuongoza hapa afrika ukiachana na hizo mbili zingine zilizotinga kumi bora afrika ni Al-Merreikh Omdurman ya Sudan nafasi ya 3 ikiwa na pointi 113.5 ikifuatiwa na Chelsea FC Berekum ya nchini Ghana 4 ikiwa na pointi 113 , Wydad Casablanca ya Morocco nafasi ya 5 ikiwa na poniti104.5 , timu nyingine ni Djoliba AS ya nchini mali, Al Ahly ya nchini Egypt, 8- Sunshine Stars ya nchini Nigeria, Desportivo Interclube ya nchini Angola na inayofunga dirisha ni timu ya Stade Malien ya nchini Mali ikiwa na pointi 81
Thursday, November 1, 2012
Gervinho nje kwa wiki 3.
GERVINHO |
Mshambuliaji wa klabu ya arsenal Gervinho atakuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki 3 kutokana na kusumbuliwa na tatizo la kifundo cha mguu(aknkle) ambapo alikumbwa na tatizo hilo wakati wa mchezo wa ligi dhidi ya QPR wiki iliyopita.Hivyo Gervunho ,Wojciech Szczesny, beki wa kushoto Kieran Gibbs pamoja na kiongo Abou Diaby wataikosa mechi dhidi ya mashetani wekendu klabu ya Manchester united huko Old Trafford jumamosi ya wiki hii. |
Uhondo wa wikii hii katika uwanja wa soka duniani.
KAGERA SUGAR. |
Kwa kuanza hapa nyumbani kutakuwa na muendelezo wa mechi za ligi kuu Tanzania bara ambapo mchezo unatazamiwa kuwa mgumu ni kati ya Klabu yak ager sugar wao watakuwa nyumbani kaitaba kucheza na maafande Tanzania prison kutoka mbeya.
kIKOSI CHA ESPARANCE |
Mechi kali zitakazochezwa wikendi hii barani Afrika kutakuwa na fainali ya kwanza ya ligi ya mabingwa barani afrika ambapo klabu ya Al Ahly itakuwa nyumbani kuikaribisha klabu ya Esparance ya nchini Tunisia
| SAINT CAZORLA |
Uko barani ulaya kubwa zaidi ni mchezo kati ya klabu ya Manchester united watakao kuwa nyumbani Old Trafford kuwakaribisha washika bunduki wa jiji la London klabu ya Arsenal huku kukiwa na maswali je,washika bunduki hao watarudisha kipigo walichokipokea msimu wa mwaka jana cha goli 8-2
ROBIN VAN PERSIE. |
Mchezo huu unatazamiwa kuwa mgumu kwa pande.pamoja na hilo mashabiki wengi wa soka watakuwa wana hamu kubwa ya kumuona mshambuliaji mahili ambaye ukipita mtaani hususani kwa mashabiki wa Manchester upenda kumuita robini magoli kutokan na umahili wake wa kufumania nyavu,swali je atamfunga mlezi wake aliyemlea hadi kufikia hapo..? dakika 90 ndizo zitakazo toa majibu ya maswali yote.
LUIS SUAREZ |
Wikendii hii tena mchezo unaotazamiwa kuwa mgumu ni kati ya majogoo wa london klabu ya Liverpool walioambulia kipigo cha goli 3-1 katika mchezo wa kuwania kombe la capital one ambapo Liverpool watakuwa nyumbani Anfield kucheza na klabu ya Newcstle
Subscribe to:
Posts (Atom)