Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Tuesday, October 30, 2012

Micha richards nje kwa wiki sita au nane


Micha Richard

   Beki wa timu ya taifa ya England pamoja na mbaingwa ligi kuu nchini uingereza  klabu ya Manchester  city  Micah Richards atakuwa nje  ya uwanja kwa takribani   wiki sita  au nane  kutokana  na  kufanyiwa  upasuaji wa goti  lake  la kulia  mara baada ya kuamia katika  mchezo wa ligi dhidi ya  klabu ya Swansea  city jumamosi ya wiki iliyopita

 Tangu kuanze  kwa ligi kuu ya nchini uingereza  Richards  amefakiwa  kucheza mechi nne za ligi hiyo hii ni kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya goti.hivyo klabu ya Manchester  city   imefiksha majeruhi  3  wanaocheza  safu hiyo ya ulinzi,wachezaji hao ni Maicon pamoja na Pablo  zabaleta.

 

Falcao: kwasasa sina mpango wa kuondoka Atletico madrid


Radamel-Falcao

Mshambuliaji mahili anayecheza  katika  klabu ya Atletico Madrid  mkolombia  Radamel Falcao   amesema  hafikirii  kuondoka   katika  klabu  hiyo  mara  baada ya kuisadia klabu yake  kupanda  hadi  nafasi ya pili  nyuma ya vinara wa ligi hiyo klabu ya Barcelona  
   "Kwasasa  Sina  mpango  wa kuondoka na wala sijawahi kufikiria  kutaka kuondoka", alisema Falcao ambaye anarekodi  nzuri ya upachikaji wa magoli kwani tangu kuanze kwa ligi ya nchini uhispania  falcao ameweza kufunga magoli 10 akiwa nyuma ya vinara wa upachikaji  magoli kin Lionel Messi mwenye magoli 13,Christiano Ronaldo akiwa na magoli 11.
Pia ikumbukwe siku kadhaa  zilizopita  kulikuwepo uvumi kuwa  mchezaji huyo anataka kujiunga  na mabingwa wa ligi hiyo klabu ya Real Madrid  ambayo inashika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo

kocha wa timu ya taifa ya zambia Herve Renard amesikitishwa na kitendo cha timu ya taifa ya kenya kumteuwa Henry Michel kama kocha wa timu ya

kocha-Herve Renard

Kocha wa timu ya taifa ya Zambia  mfaransa  Herve  Renard  ameshangazwa  na kitendo  cha timu ya  taifa ya Kenya Harambee  stars  kumteuwa mfaransa  mwenzake  Henry  Michel  kama kocha mkuu wa timu hiyo

Kocha huyo amesema Henry  Michel  si chaguo sahihi  kwa  timu ya taifa ya Kenya  kwani ni vema  kwa timu ya taifa ya kenya kupata kocha ambaye ataendana na wachezaji ikiwemo kuwapa hamasa ya kucheza mpira

 “Kenya  ina kila kitu  lakini  nafikiria ya kwamba imekosea kuchagua kocha ambaye  hana atauwezo  wa kuisaidia timu  kwani Henry  Michel  rekodi yake ni mbaya    hivyo   kenya inahitaji    kocha   ambaye anauwezo mkubwa wa kufundisha na sio Henry”,Alisema  kocha Herve Renard.

Herve  Renard ni kocha  mwenye  mafanikio makubwa katika timu ya taifa ya Zambia kwani amefanikiwa kutwaa  kombe la mataifa ya afrika maarufu kama (AFCON)  mwaka huu wa 2012 akiifunga timu ya taifa ya ivory cost kwa mikwaju ya penaiti,pia kocha huyo amefanikiwa tena kuipeleka Zambia katika michuano hiyo itakayofanyika huko nchini Afrika kusini mapema mwakani

 

Stewart kurejea kuinoa klabu ya Azam


kocha Stewart-Hall

Kocha wa zamani wa klabu ya Azam  Stewart  Hall  ambaye alijiunga klabu ya Sofa paka ya nchini Kenya  anatazamiwa kurudi kukinoa kikosi chake cha zamani cha Azam mara baada ya kushindwa kukubaliana   na  klabu ya Sofa paka

Stewart amesema  anarudi  nchini Tanzania  katika klabu yake ya zamani  kwani klabu ya azam imemuomba msamaha kwa yale yote yaliyotokea.

 Hivyo stewart ataingia nchini Tanzania siku ya jumatano majira ya  usiku kwa ajiri ya kuja kuitumikia klabu yake ya zamani ya azam ambayo tayari imekwisha kumfukuza mrith wa Stewart hall   kocha  Boris Bunjak kutokana na kiwango kibovu kinachooneshwa na klabu hiyo  ikiwemo kupoteza michezo yake ya ligi kuu Tanzania  bara.

Kocha Stewart  akiwa  katika klabu ya sofa  paka amefanikiwa kushinda mchezo mmoja wa ligi,akipoteza michezo 2 na kutoa sare  michezo 2.

Stewart   Alipokuwa katika klabu ya azamu kabla ya kutupiwa virago  kocha huyo alifanikiwa kuipatia klabu ya azamu  kombe la  mapinduzi, kushika nafasi ya pili katika michuano ya Urafiki,ligi kuu Tanzania  bara pamoja na michuano ya kuwania kombe la kagame.

 

kwa hali hii...Tutamaliza makocha wote bila hata mafanikio

kikosi cha  Azam

Klabu ya  Azama  maarufu  kama  wanaramba ramba  imetangaza rasimi kumfukuza  kocha wake Boris  Bunjak kufutia  matokeo mabaya  katika  michuano ya ligi kuu Tanzania bara

Kwa mujibu wa Afisa  habari wa klabu hiyo  Patrick  Kahemela  amesema ni kweli kocha huyo amerushiwa virago kutokana na kuwa na matokeo  mabaya ikiwemo hata kiwango kibovu kinachooneshwa  na  klabu hiyo kitu ambacho kinapelekea kupoteza kwa michezo yake na hivyo kujikuta klabu hiyo ikishuka hadi nafasi ya nne kutoka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara

 

Boris-Bunjak

Kocka huyo anatazamiwa  kuondoka nchini  Tanzania  kulekea  nchini kwao siku ya alhamisi ya wiki hii huku kunatetesi kuwa  kocha aliyetimuliwa  Stewart  Hall ndiy atakayekuja kukinoa kikoso hicho

Rekodi ya  Bunjak  tangu ajiunge  na klabu ya azam  amefanikiwa kushinda  mechi nne, kutoa sare mara 3,na kupoteza  michezo 2 huku mchezo wa simba ndio uliopelekea kocha huyo kufungishiwa  virago  mara baada ya kupokea kipigo cha goli 3-1

 

Hizi  ni mechi ilizocheza klabu ya Azam  ikiwa chini ya kocha Bunjak kabla ya kutimuliwa.

Azam 1-0 Kagera Sugar

Azam 2-2 Toto African

Azam 3-0 JKT Ruvu

Azam 1-0 Mtibwa Sugar

Azam 1-0 African Lyon

Azam 1-0 Polisi Morogoro

Azam 0-0 Prisons

Azam 1-1 Ruvu Shooting

Azam 1-3 Simba