Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Thursday, October 25, 2012

Roberto Mancini amekata tama ya kusonga mbele katika michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya.

Roberto Mancini



Kocha wa klabu ya manchester  city muitaliano Roberto Mancini amekata tamaa na kusema kuwa timu yake kubaki katika michuano  ya ligi ya mabingwa  barani ulaya   itakuwa ni maajabu.

Kauli hiyo imekuja Kufuatia  klabu ya Manchester city kupoteza  mchezo wake  dhidi ya klabu ya Ajax  kwa kuambulia kipigo cha goli 3-1 katika michuano ya  ligi ya mabingwa barani ulaya(UEFA)

     Roberto Mancini, “Ni ngumu sana kwa sababu kuna timu zenye pointi 7,nyingine pointi 6,pointi 3 hivyo itakuwa ni maajabu kuendelea kwa hatua inayofuata”
Akizungumizia hali ya mchezo Mancini amesema timu yake ilicheza vibaya kulinganisha wa wenyeji wao timu ya Ajax.

      “ Tumecheza mpira wenye kiwango kibovu,tumepata nafasi chache lakini tumeshindwa kufunga  kutokana  na kiwango kibovu cha walichoonesha wachezali”,alisema kocha Roberto Mancini.

JOE- HART akiwa amelala baaada ya kumalizika kwa dk 90 huku wakiwa wamefungwa goli3-1

Katika kundi D klabu ya Manchester city ndio inayoshikilia mkia ikiwa na pointi 1 huku vinara wa kundi hilo ni mabingwa ligi ya ujerumani klabu ya Borussia Dortmundi yenye pointi 7.

No comments:

Post a Comment