Luis SuarezChama cha soka cha nchini Uruguay kimetangaza kutokuwa na imani na Jim Boyce ambaye ni makamu wa rais wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA na kuiomba bodi ichunguze tabia ya Jim BoyceHatua hii imekuja kufutia siku chache zilizopita makamu huyo kumshutumu mchezaji wa Taifa hilo Luis Suarez kwa kitendo chake cha kujiangusha ndani ya eneo la penaiti ili apewe peanaiti ambapo suarez alifanya hivyo wakati wa mchezo wa ligi kuu nchini uingereza dhidi ya timu ya stoke city.
Barua iliyotumwa na chama chama cha soka cha Uruguay katika shrikisho la mpira wa miguu duniani FiFA inalalamikia kitendo cha makamu huyo kutaka kuendeleza chuki na uhasama miongoni mwa wachezajiPia barua hiyo inaeleza kwamba kwa mujibu wa sheria na kanuni za shrikisho la mpira wa miguu duniani FIFA linamtaka kila kiongozi ndani ya shikisho hilo kuheshimu taratibu zilizopangwaHivyo kutokana na makamu huyo kukiuka moja ya sheria hizo Chama hicho cha soka cha ya Uruguay kimetangaza kuwa hakitatambua nafasi yake kama kiongozi ikiwemo kutokuwa na imani naye kwani anachochea chuki miongoni mwa wachezaji. |
Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo
Friday, October 12, 2012
Chama cha soka cha Uruguay kimesema hakina imani na makamu rais wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA, Jim Boyce
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment