Timu Yanga |
Klabu ya soka ya mpira wa miguu nchini Tanzania,klabu ya yanga maarufu kama vijana wa jangwani leo hii kupitia kamati ya wazee hiliyokaa tarehe 6.10.2012 kujadiri hatima ya klabu hiyo kuhusu kuvaa nembo yenye rangi nyekundu hatimaye wazee hao wametoa tamko kuhusiana na suala hilo na kusema wako tayari kucheza ligi ya Tanzania visiwani,au michezo mingine kama mchezo wa bao kuliko kuvaa jezi yenye nembo nyekundu.
Ibrahim-Akilimali-katibu wazee Yanga |
Akiongea na waandishi wa habari leo hii jijin dare s salaam katibu wa wazee wa klabu hiyo Ibrahim Akilimali amesema wanaishangaa kampuni ya simu ya Vodacom kwa kubadilika badilika kwani mwaka jana Vodacom ilikubali ombi la klabu hiyo na kuweka nembo nyekundu,mwaka imkuwaje kwa kampuni hiyo kugeuka..?
Ilikuhakisha kamati hiyo ya wazee ya klabu hiyo imeamua kuwakubusha wanachama,kampuni ya simu ya Vodacom kuwa mnamo mwaka 1955.22.08 wakati huo mdhamini wa klabu hiyo alikuwa ndugu Abdallah Keremji,nchini ya uongozi wa Mzee kondo s. kipwata
Kumbukumbu ni kwamba mwaka huo kuliandaliwa mechi kati ya klabu ya Yanga dhidi ya timu ya mabaharia ,mgeni rasimi wa mchezo huo alikuwa Gavana Edward Twining.
Timu hiyo ya mabaharia ilikuja na jezi zao nyekundu ili kuwapa yanga wazivae mbele ya Mgeni rasimi lakini timu ya Yanga ilikataa na kusema wako tayari kucheza kifua wazi kuliko kuvaa jezi nyekundu
Vijana wa Yanga-Tegete,Niyonzima na Chuji |
No comments:
Post a Comment