Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Tuesday, October 16, 2012

Marcelo nje miezi mitatu.

Marcelo - Brazil

Marcelo   viera

Mchezaji wa mabingwa wa ligi kuu ya nchini uhisipania  pamoja na timu ya taifa ya brazili Marcelo viera da Silva Júnior   huenda akaa nje ya uwanja kwa takribani  miezi mitatu kufuatia kuumia  mguu  wakati  wa mazoezi katika timu yake ya taifa ya brazili

Chama cha soka  cha nchini  brazili kimethibisha kuumia kwa mchezaji huyo na kusema kuwa ameumia kifundo cha mguu(ankle) hivyo kutokana na tatizo hilo huenda Marcelo akanyiwa upasuaji mda si mrefu

Kwa upande  wake Marcelo amesema anaamini atapona na kuahidi kuwa atarejea uwanjani mda si mrefu kabla  kwa ajiri ya kuitumikia  timu yake ya taifa ya brazili.

Mchezaji huyo (24 )hucheza nafasi ya beki wa kushoto katika klabu ya real Madrid kwa sasa atakuwa amempa wakati mgumu kocha mreno jose morinho kuchagua nani atakayecheza nafasi hiyo  pindi timu hiyo itakapocheza dhidi ya Celta Vigo jumamosi hii  kwani mchezaji ambaye angechukua nafasi hiyo  mreno Fabio Coentrao yuko nchini kwao kuitumikia timu yake ya taifa ya ureno kwa ajiri ya michezo ya kufuzu kuelekea brazili mwaka 2014
 

 

No comments:

Post a Comment