Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Tuesday, October 30, 2012



ENDAPO HII TIMU IKIUNDWA KUWA TIMU MOJA ITAKUWA BONGE LA TIMU.

Wachezaji bora   wa mwezi wa kumi wanaounda kikosi cha kwanza   cha wachezaji  kumi na moja ambao wameonyesha kiwango cha juu kwa kuzisaidia timu zao  kupata ushindi katika michezo ya ligi kuu Tanzania bara  mwezi huu wa kumi ni  wachezaji hao ni
1.Golikipa
Yaw   berko
2.Mabeki
Shomari kapombe, mbuyu twite,stephano mwasika,saidi choro,
3.Viungo
Mwinyi kazimoto,Haruna niyonzima,amri kiemba,
4.Washambuliaji
Edward  Christopher,Emanul Okwi,

Ukianza kuangalia kiwango cha mchezaji mmoja mmoja kati ya hawa bila shaka hutokuwa na wasiwasi hata kidogo kwani wachezaji hawa wameonyesha kiwango cha hali ya juu  katika michezo mbalimabli ya ligi kuu Tanzania bara  tangu kuanze kwa mwezi huu wa kumi,

Christopher Edward


Mchezaji kama Edward Christopher  ni mchezaji mwenye umri mdogo ukilinganisha na wachezaji kama vile kina tegete,Emanuel okwi,said bahanuzi ambaye amejipatia jina katika michuano ya kagame iliyofanyika mwaka huu hapa nchini Tanzania.

Pamoja na kuwa na umri mdogo kocha milovan cirkovic ameamua kumpa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza hii ni kwasababu anajua kuwa Christopher anauwezo mkubwa wa kumiliki mpira,kufunga,kwa mfano wakati wa  mchezo wa maasimu wa jadi Simba na   Yanga kila mmoja hakutegemea kama christoper angestahimili kasi ya wakubwa zake,kuipa wakati mgumu ngome ya Yanga.
 
Hivyo   Christpher Edward ni mmja ya washambuliaji wazuri hapa Tanzania na akitulia,akafanya kazi kwa bidiii huku akiwa na malengo akilini mwake basi na yeye atafanikiwa kufuata nyao  za matanzania mwenzake Mbwana Samatha.
Kwa upande wa viungo sio siri wachezaji hawa wanafanya kazi.kiasi kwamba unapokuwa uwanjani alafu timu moja wapo ya wachezaji hawa iko nyuma kwa goli kadhaa utaona ni jinsi gani wanavyokuwa wanahaha kwa kutafuta mpira,kutengeneza mazingira ya kufunga na hata kutafuta nafasi ya wao kufunga   wao wenyewe.

Mwinyi kazimoto ambaye waweza sema ndio tegemeo kubwa kwa timu ya simba kiasi kwamba akiumia mashabiki na hata baadhi ya viongozi hupatwa  na wasiwasi mkubwa  wa nani atayeziba pengo hilo

Haruna   Niyonzima(Fabrigas wa afrika mashariki) hapa kwa wanayanga huwaelezi kitu chochote kuhusu kiwango cha Haruna ambaye si dhani timu ya yanga inaweza kumuuza kiurahisi amekuwa na mchano mkubwa sana katika safu ya kati ya timu ya Yanga.

Mbuyu Twite

Katika safu ya ulinzi hapo haina shida kwa kunavijana ambao wanajua wanachokifanya.mchezaji kama mbuyu twite ambaye alileta utata katika usjiri wa kuichezea timu Yanga naye pia  ameonesha kiwango cha juu.kwa  mfano katika mechi ya maasimu wa jadi simba na yanga sio siri Twite alionesha kiwango cha  juu zaidi,

shomari kapombe   ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa  wa kucheza  nafasi zaidi ya moja uwanjani. Kwa mfano katika mchezo wa ligi kati ya Timu ya Simba na Maasimu wa wakubwa Timu ya  Yanga  mwanzo mwa mwezi huu  shomari alionesha uhodaro mkubwa wa kuwahimli  washambuliaji wa Yanga kama  vile  Saidi Bahanuzi ambaye  ni moja ya wachezaji wasumbufu ,wenye nguvu  ambao uhitajika umakini  katika kuwakaba lakini siku hiyo  shomari kapombe alifanya kazi ya ziada.

Kwa upende wa golini hapo haina shida kwani mghana  berko ni moja ya golikipa wazuri katika ligi kuu   Tanzania  bara  licha  ya kuwa anasumbuliwa na majeruhi lakini bado anaonesha  umahiri wake




Thursday, October 25, 2012

AFCON 2013, Je zambia itatetea ubingwa....?

Zimebakia takribani siku 86 kwa wapenzi wa soka barani Afrika na duniani kuelekea Bondeni kwa mzee Mandela ambako michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika (AFCON) itafanyika huku ile droo ya makundi imekwishafanyika na kushuudia mabingwa wa kombe hilo timu ya taifa ya Zambia ikiwa kundi moja na timu ngumu ya Nigeria,burkinafaso pamoja na Ethiopia.

 


Makundi ya timu zitakazoshiriki michuano hiyo ni

Group A: South Africa, Morocco, Cape Verde, Angola

Group B: Ghana, Mali, Niger, DR Congo

GROUP C: Zambia, Ethiopia, Burkina Faso, Nigeria

Group D: Ivory Coast, Togo , Algeria, Tunisia

Katika makundi haya kundi linalotazamiwa kuwa  gumu ni kundi D pamoja na kundi B kwani makundi haya mawili yamebeba timu kongwe na ngumu.kwa mfano kundi D lenye timu za ivory cost ambao walikosa ubingwa huo mwaka huu kwa kufungwa na timu ya Zambia kwa njia ya peniti.


Timu ya taifa ya Afrika kusini

 Timu ambayo inayotazamiwa kuleta upinzani katika kundi hili ni timu ya taifa ya Tunisia,pamoja na hawa Algeria ambapo kwa kawaida timu hizi za mafia za kiarabu zimekuwa zikileta ugumu kwa timu hizi za asili za kiafarika.

 Katika kundi B hili nalo ni kundi gumu zaidi kwani limekutanisha timu ngumu kama Mali,DR Congo ambapo timu kama ya Ghana inauchu mkubwa sana wa kutwaa taji hili.

timu ya taifa ya zambia

Bingwa mtetezi yeye katika kundi lake si gumu sana pengine ukilinganisha na kundi A kwani Zambia hatapata upinzani mgumu kama atakaopata  Ghana itakapocheza na Mali au congo ila ugumu utakuja pindi Zambia atakpocheza na timu ya taifa ya Nigeria 

 

Hata Ethiopia,Burkinafaso, si timu za kubeza kwani nazo zimejianda vya kutosha katika kuelekea huko afrika kusini. 

Didier Drogba.

Swali je, Zambia itatetea ubingwa wake,Didier drogba yuko tayari kuona anakwenda kusitaafu soka bila hata ya kulipatia taji taifa lake la ivory cost…?

MORINHO:BAADHI YA MAKUNDI LIGI YA MABINGWA ULAYA NI VIBONDE

JOSE MORINHO
Mreno jose morinho mara baada ya kushuudia timu yake ikiondoka uwanjani signal iduna park kwa kichapo cha goli 2 -1  kocha huyo mwenye maneno mengi  amesema baadhi ya makundi katika michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya kuwa ni makundi yasio magumu(joke)


Morinho ambaye yuko katika kundi linalosadikiwa kuwa ni kundi gumu kuliko yote  likiwa na timu kama vile mabingwa wa ujerumni Borussia Dortimundi,Ajax pamoja na timu ya manchester city ambao wameonekana kuwa ndo vibonde wa kundi hilo amesema kwamba

   “Hili ndo kundi gumu kuliko yote.kuna baadhi yao si magumu kama vile kundi lenye timu ya  BATE Borisov  ya nchini Beralus”.

Akielezea nafasi ya timu yake kusonga mbele katika kundi hilo morinho amesema  bado kuna nafasi kwa kila timu ila kilichopo kwa sasa ni kujianda kwa ajiri ya mechi za marudiano

Roberto Mancini amekata tama ya kusonga mbele katika michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya.

Roberto Mancini



Kocha wa klabu ya manchester  city muitaliano Roberto Mancini amekata tamaa na kusema kuwa timu yake kubaki katika michuano  ya ligi ya mabingwa  barani ulaya   itakuwa ni maajabu.

Kauli hiyo imekuja Kufuatia  klabu ya Manchester city kupoteza  mchezo wake  dhidi ya klabu ya Ajax  kwa kuambulia kipigo cha goli 3-1 katika michuano ya  ligi ya mabingwa barani ulaya(UEFA)

     Roberto Mancini, “Ni ngumu sana kwa sababu kuna timu zenye pointi 7,nyingine pointi 6,pointi 3 hivyo itakuwa ni maajabu kuendelea kwa hatua inayofuata”
Akizungumizia hali ya mchezo Mancini amesema timu yake ilicheza vibaya kulinganisha wa wenyeji wao timu ya Ajax.

      “ Tumecheza mpira wenye kiwango kibovu,tumepata nafasi chache lakini tumeshindwa kufunga  kutokana  na kiwango kibovu cha walichoonesha wachezali”,alisema kocha Roberto Mancini.

JOE- HART akiwa amelala baaada ya kumalizika kwa dk 90 huku wakiwa wamefungwa goli3-1

Katika kundi D klabu ya Manchester city ndio inayoshikilia mkia ikiwa na pointi 1 huku vinara wa kundi hilo ni mabingwa ligi ya ujerumani klabu ya Borussia Dortmundi yenye pointi 7.

Monday, October 22, 2012

Wenger hasikitishwa na mwenendo mbaya wa timu yake katika ligi kuu ya nchini uingereza


Arsene Wenger

Kocha wa  washika bunduki wa London klabu ya arsenal mwenye uraia wa ufaransa ARSENE WENGER amesema hafurahishwi na kikosi chake kupoteza michezo muhimu katika ligi kuu nchini uingereza kwani kitu hicho kinaifanya klabu hiyo kuwa katika nafasi mbaya katika msimamo wa ligi na ata na ata kuacha nafasi kubwa dhidi ya klabu ambayo inaongoza ligi hiyo kwa sasa.

Arsenal ambayo iko katika nafasi ya tisa ilipata pigo baada ya kupokea kichapo cha goli moja kwa yai kutoka kwa klabu ya Norwich city siku ya jumamosi na kuifanya klabu hiyo kuwa nyuma kwa point kumi dhidi ya vinara wanaongoza ligi klabu ya Chelsea almaarufu kama the blues.

Mwanidishi:  Frank momanyi mgunga