Karibu katika dira ya michezo kwa habari motomoto za michezo ya ndani na nje ya nchi
Karibu katika dira ya michezo

Sunday, September 23, 2012



             UONGOZI WA YANGA WAMTIMUA KOCHA WAKE

Uongozi wa klabu ya sokaya Yanga umesitisha mkataba wa kocha wake mkuu Tom Saintfiet pamoja kuwaengua katibu mkuu ,meneja pamoja na msemaji wa klabu hiyo yenye maskani yake makutano ya mitaa ya twiga na jangwani 

aliyekuwa kocha wa Da Young African -Tom Saintfiet

 

Ilikuwa hali ya shamra shamra kwa wanachama na mashabiki wa  klabu ya Yanga wakati wakati wakimpokea kocha Tom Saint fiet kuja kuchukua nafasi ya Kostadin Papic aliyetimuliwa kikosi hapo zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kumalizika kwa ligi kuu msimu uliopita

Maisha ya kocha Tom Saitfiet  klabuni hapo yamedumu kwa miezi miwili tu  baada ya uongozi wa klabu hiyo kusitisha  mkataba na kocha huyo raia wa ubelgiji  kutokana  na kushindwa kuendana na mipango ya klabu hiyo 



Makamu mwenyekiti  wa wanajangwani Clement Sanga amedai kuwa uongozi umefikia hatua ya kusitisha mkataba na kocha huyo  kwa kuwa ameshindwa kusimamia mipango ya klabu  ambapo alikataa timu kuiweka kambini muda mrefu  na badala yake kutaka ikae siku tatu kabla ya mechi 

Uongozi huo umempa majukumu ya ukocha mkuu Fred Felix Minziro kwa sasa mpaka atakapopatikana kocha mwingine atakayekinoa kikosi hicho
 

aliyekuwa katibu wa YANGA-Celestine Mwesigwa

 Katikamabadiliko hayo pia uongozi umemtangaza mchezaji wa zamani wa klabu hiyo Lawrence Mwalusako kukaimu nafasi ya katibu mkuu baada ya kusimamishwa  kwa aliyekuwa katibu wa timu hiyo Celestine Mwesigwa huku  Denis Oundo akiteuliwa kuwa mkurugenzi wa fedha na utawala

Wana wa Jangwani  YANGA

Tom Saintfiet amedumu katika kikosi cha Yanga kwa muda wa miezi miwili tu baada ya kutimuliwa kwa  kocha Kostadin   Papic aliyechukua mikoba ya mganda Sam Timbe  ambaye naye alitimuliwa kikosini  hapo baada ya kukaa na kikosi hicho na kutwaa ubingwa wa ligi kuu 

No comments:

Post a Comment